Tabu Zangu

Haleluya naitazamia mbingu mpya na nchi Mpya
Huko nitapumzika milele
Tabu zangu zikiisha, nitamwona Bwana wangu
Akinikaribisha kule, karibu upumzike
Hapa ndipo nyumbani kwako, hapa ndipo Mahali pako
Hapa ndipo makao yako, karibu upumzike
Haleluya nitaketi kwa furaha, nitapumzika kwa Mungu, nitapumzika
Nitavikwa mavazi meupe, nitavikwa taji ya Ushindi
Tabu zote na mateso yote, hakika vitakoma
Nitaungana na malaika, maserafi na makerubi
Tukiimba nyimbo za ushindi, haleluya usifiwe
Naona mbingu zimefunguka, na Yesu yu mkono Wa kuume
Akinitazama kwa upole, kwa macho yenye Huruma
Naona mbingu zimefunguka, na Yesu yu mkono Wa kuume
Akinitazama kwa upole, kwa macho yenye Huruma
Tatazama vidonda vyangu, tatazama makovu Yangu
Niloumizwa duniani, na watu wa ulimwengu
Tatazama vidonda vyangu, tatazama makovu Yangu
Niloumizwa duniani, na watu wa ulimwengu

Tachukua kitambaa, atanifuta machozi
Akisema pole mwanangu, Yesu tanikumbatia
Bado kitambo kidogo, nitapumzika
Yesu atanipeleka, kwenye kijito cha uhai
Huko taniosha mwili wangu, nitapewa mwili Mpya
Nami nitaimba hosana, hosana ndiye mbarikiwa
Nitaruka kama ndama, milele hata milele
Yesu atanipeleka, kwenye kijito cha uhai
Huko taniosha mwili wangu, nitapewa mwili Mpya
Nami nitaimba hosana, hosana ndiye mbarikiwa
Nitaruka kama ndama, milele hata milele
Oh Baba Tavumilia, kwa ajili yako Baba
Yatosha walivyokuonea, Yatosha Walivyokudhulumu
Yatosha walivyokupiga, karibu upumzike
Yatosha walivyokuonea, Yatosha Walivyokudhulumu
Yatosha walivyokupiga, karibu upumzike
Yatosha walivyokuudhi, Yatosha Walivyokutukana
Yatosha walivyokuzomea, karibu upumzike
Yatosha walivyokuudhi, Yatosha Walivyokutukana
Yatosha walivyokuzomea, karibu upumzike
Haleluya, mateso yangu yakiisha nitauona uso Wa Mungu
Nitamwona Yesu niliyepigwa kwa ajili yake
Yatosha walivyokuonea, Yatosha Walivyokudhulumu
Yatosha walivyokupiga, karibu upumzike
Yatosha walivyokuonea, Yatosha Walivyokudhulumu
Yatosha walivyokupiga, karibu upumzike
Yatosha walivyokuudhi, Yatosha Walivyokutukana
Yatosha walivyokuzomea, karibu upumzike
Yesu atanipeleka, kwenye kijito cha uhai
Huko taniosha mwili wangu, nitapewa mwili Mpya
Baada ya tabu, ni furaha



Credits
Writer(s): Rose Muhando, Anastacia Mukabwa
Lyrics powered by www.musixmatch.com

Link