Like Father, Like Son

YogoWaMasoja

Aaah

Hii ni kwa taifa la kesho
Like father like son
Acha tu-take care

No 1

(YogoWaMasoja)

Nataka kuteta nawe,
Nataka kusema nawe,
like father like son,
nyota inayong'aa mrithi wangu maishani,
jembe la thamini isiyopimika kwa mizani,
juu zaidi ya madini zaidi ya nuru gizani,
ulizaliwa kwa uchungu utatunzwa kwa jasho langu,
ndiyo maana naenda mbio kutwa nzima sionekani,
niko busy nina-hustle natafuta maisha fulani,
nikulishe kinda langu nikuvishe,
nahangaika nikutunze mwanangu nikusomeshe,
u-takeover harakati uziendeleze,
mama yako umtunze tafadhari usituangushe,
kuwa makini usijetekwa na mitaa,
ukashika masilaha na kufanya mabalaa.

(Leah)

Like father like son,
nakwambia kama utani,
maneno haya usipuuze,
ili ndoto zako utimize,
ukivamia maisha lazima utafeli,
dunia ya sasa imejaa utapeli,
maneno haya usipuuze,
like father like son.

No 2

Najuwa unanimiss, mishemishe kutwa nzima naenda lesi,
aah aah usijesema nakugaya,
i'm a good father najuwa ku-take care,
dady is back home gift zako njoo pokea,
umechafuka unajifunza ukiniona usiniogope,
njoo niku-hug wala sitojari tope,
samaki mkunje angali bado mbichi,
ukisubiri akauke anakatika hakunjiki,
hakuonei mama akikukalipia,
ikibidi anakuchapa kurekebisha tabia,
uwe stable darasani na nyumbani,
nakagua daftari nafika mpaka shule kujua habari zako,
ukifeli naumia na hasira zaidi ya mbogo,
sitishiki siogopi ukisema dingi ni mnoko.

(Leah)

Like father like son,
nakuambia kama utani,
maneno haya usipuuze,
ili ndoto zako utimize,
ukivamia maisha lazima utafeli,
dunia ya sasa imejaa utapeli,
maneno haya usipuuze,
like father like son.

No. 3

(YogoWaMasoja)

Cheza mbali na hatari,
mitaa imechafuka hali bado siyo shwari,
wakora wanavinjari,
nani wa mpotoshe wa mpotezee mbali,
watu wamekosa imani,
anajifanya mwema anakuweka matatani,
gold digger drug dealler wamejaa mitaani,
wakabaji waporaji wanatunyima amani.

(Leah)

Sitaki sema maneno mengi,
ikawa kama na kulaani,
jichunge maradhi ni mengi,
usijeondoka na HIV,
kazana kwanza na shule (eeh),
starehe utafanya baadae,
wengi wenye haraka mpaka sasa hawajafanikiwa.

(Leah)

Like father like son,
nakwambia kama utani,
maneno haya usipuuze,
ili ndoto zako utimize,
ukivamia maisha lazima utafeli,
dunia ya sasa imejaa utapeli,
maneno haya usipuuze,
like father like son.

Outlaw.

(YogoWaMasoja)

(Aah), Leah,
yogowamasoja,
(aah) Gkifaa,
like father like son,
yeah, i'm out.



Credits
Writer(s): Ramon Rivera
Lyrics powered by www.musixmatch.com

Link