HipHop (feat. Sam Kisser)

GuruMc
Naswali kwako mrembo wangu naye kupenda
Hivi ni kweli bado unanipenda hutonitenda
Maana nilichelewa kutambua nakupenda
Si unajua utoto mwingi apo golini na machenga
Nilianza kupenda ndo kwanza sijabalehe
Mama hakupenda kuniona nkitoka mimi na we
Cha ajabu hukunitenda kwa siri ukaja tuonge
Mama anakupenda kweli ila penzi wacha Tushare
Miaka ikapita ata sijui njia gani
Skendo ikatoka eti unawalisha mamijan
Mara wengine unga kweli wewe kisirani
Ila bado nakupenda ivo ivo kwani gani
Niliwatolea mademu waloleta shobo
Hawakujua kuwa na demu mtoto wa kigogo
Demu mwenye figure demu flani asiye na nyodo
Ila paka leo sijui ka nibonge ama model
Nachomsifu huyu demu sio kicheche
Hazuzuki na pesa majina wala uchebe
Hazungukwi na wenye fitina wivu na wenge
Pigo zake na mabeat mamtoni ama vilinge
Nilimkuta na Nash pale KINASA
Anavyopenda shule akatoka na Darassa
Mara Fid Songa Killer mpaka Nacha
Na anasema tupo wengi anatupenda mpaka sasa
Mwisho wa mwezi Arusha anakwenda SUA
SAUTI YA MTAA kwa NextTz alitua
Anapenda kwenda mwanza GOGOVINU c mnaijua
DDC CHIMBUKA yan Dom city anaijua
Namshangaa Madee kusema demu halipi
Anachosema demu madee hamridhishi
Akamwambia waachane ili mambo yawe fiti
Mr Blue akasikia akasema baki na mimi

Chaka kila chaka niko naye staki kumpoteza yeye
Anavowakawaka noma
Ilo body lake choma
Niko naye kila kona
Say Ei ebwana nomaaa yeeye nomaa yeeye
Ebwana nomaa yeeye nomaaa yeeye
Ebwana nomaa yeeye (Minatapa nkiwa naye) nomaa yeeye (Ananifany wanikome)
Ebwana nomaa yeeye (Me nang'ara nkiwa naye) nomaa yeeye (Kila kona wanisome)

Marekani alitumika vizuri akaleta uhuru
Watu weusi heshima ikapanda wakawa huru
Amekua ajira vijana kawanusuru
Kweli na demu bora usimfananishe na lulu
Kazi zake ni nyingi uyu demu anawakilisha
Jamii nzima paka mademu anawafundisha
Kuhusu biashara siasa maisha ana elimisha
Rika zote anamisingi ase usije pindisha
Akitumika vizuri huwa anasema ukweli
Hafichahi mabaya cha msingi uwepo ready
Nakumbuka kaka Roma alichofanywa kudadek
Dunia nzima inamtambua huyu demu ni mdediri
Popote anapofika wanakaa wanahanya
Maana sivyo alivyoumbika yani vitu anavyofanya
Uwezo wa kubadili yana hasi kuwa chanya
Dakika moja ty ukimpa anaweza akateka kaya
Vingi ni wingi na vingi vyake vigingi
Usiku na mchana kazi na kazi kazi zake ni nyingi
Siku na wiki ngazi to ngazi anapanda kingi
Na cha ajabu hapandi dau nachomsifu huwa havimbi
Bunduki risasi kama haipo basi ovyo
Mikuki mikasi usilete izo local
Na speed ni kasi usidanganywe na machoko
Ni maneno yake huwa ananamby tukiwa chocho
Unashangaa nini uyu demu wetu sote
Moyo wake hauna kimo ukitaka twende wote
Maana bado anawahitaji chipukizi kama wote
Na wote tuseme sasa Hiphop kote

Chaka kila chaka niko naye staki kumpoteza yeye
Anavowakawaka noma
Ilo body lake choma
Niko naye kila kona
Say Ei ebwana nomaaa yeeye nomaa yeeye
Ebwana nomaa yeeye nomaaa yeeye
Ebwana nomaa yeeye (Minatapa nkiwa naye) nomaa yeeye (Ananifany wanikome)
Ebwana nomaa yeeye (Me nang'ara nkiwa naye) nomaa yeeye (Kila kona wanisome)



Credits
Writer(s): Bruno Bruno
Lyrics powered by www.musixmatch.com

Link